Ad (728x90)

Tuna Develop/Design Blog & Website & Android Application ......0717331293

Wednesday 5 April 2017

Filled Under: ,

KANISA LA WAADVENTISTA WASABATO JIMBO LA KUSINI MASHARIKI MWA LINAKABILIWA NA CHANGAMOTO ZA MILA NA DESTURI ZA MIONGONI MWA WANAJAMII KATIKA KUFANIKISHA UTUME WA INJILI.

MAKANISANI ZA KITAIFA
UBUNGO PLAZA -UKUMBI AMBAO MIKUTANO YA MAWASILIANO UNAOENDESHWA NA JIMBO LA KUSINI MASHARIKI MWA TANZANIA INAFANYIKA           



Kanisa la waadventista wasabato jimbo la kusini mashariki mwa tanzania linaloundwa na mikoa ya lindi, mtwara pwani pamoja na dar es salaam linakabiliwa na changamoto za mila na desturi zac miongoni mwa wanajamii katika kufanikisha utume wa injili.

Hayo yameelezwa na katibu wa jimbo la kusini mashariki mwa Tanzania mch. TOTO NDEGE BWIRE KUSAGA wakati akizungumza na morning star radio katika ukumbi wa ubungo plaza kwenye mkutano wa mawasiliano unaoendeshwa na jimbo la kusini la mashariki mwa Tanzania.

Aidha Mch,Toto amesema kuwa pamoja na juhudi zinazofanywa jimbo hilo bado swala la mila na desturi limeendelea kuwa changamoto kwani wanakumbatia mila ambazo ni kinyume na Imani ya kanisa la waadventista wasabato.

Pamoja na hayo ameongeza kuwa mikoa ya mtwara na lindi inahitaji kupatiwa elimu ya ujasiliamali ili kuondokana na umasikini unaotawala miongoni mwao.

Huu ni mkutano wa Tatu na wa mwisho kuendeshwa na majimbo yaliyopo ndani ya Jimbo kuu la Kusini mwa Tanzania ambapo mikutano kama hiyo imeendeshwa na Jimbo la Mashariki kati mwa Tanzania na Jimbo la Nyanda za juu kusini.

Unknown

Author & Editor

Naitwa Prince Emanuel, ni mtangazaji na muandaji wa vipindi kupitia Morning Star Radio na Morning Star Televesion Tanzania.

0 comments:

Post a Comment

 

Copyright © UNCLE PRINCE ™ is a registered trademark.
Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.