Ad (728x90)

Tuna Develop/Design Blog & Website & Android Application ......0717331293

Friday, 29 April 2016

Filled Under: ,

Katibu wa Baraza la Elimu nchini Kenya,Fred Matiangi ameonya kuwa serikali haitaruhusu kuona taasisi za Elimu zikiwalazimisha Wanafunzi wa Kiadventista kwenda shule siku ya sabato nchini humo.

MAKANISANI ZA KITAIFA



Katibu wa Baraza la Elimu nchini Kenya,Fred Matiangi  ameonya kuwa serikali haitaruhusu kuona taasisi za Elimu zikiwalazimisha Wanafunzi wa Kiadventista kwenda shule siku ya sabato nchini humo kwani ni kinyume cha mafundisho ya Kanisa la Waadventista Wa Sabato.

Matiangi amesema wanafunzi wa kiadventista nchini humo wanapaswa kupewa kipaumbele na kuwataka viongozi wa taasisi za elimu nchini humo kutotoa mafunzo ya ziada siku ya sabato ili kutowanyima wanafunzi wa kiadventista haki yao ya kuabudu,huku akisisitiza kuwa serikali ya Kenya itahakikisha jambo hilo halifanyiki.

Pia ametoa tahadhari kwa walimu wa taasisi za elimu  kutowaruhusu wahubiri  wanaotembelea taasisi hizo kwa kuwa wana ajenda zao binafsi.

Matiangi amesema utafiti umebaini kuwa baadhi ya wahubiri wamekuwa wakiwashawishi wanafunzi kujiunga na taasisi ambazo hazijasajiliwa na zenye ajenda binafsi zisizojulikana.

Asilimi 82.6 ya idadi ya watu nchini Kenya ni waumini wa Madhehebu ya Kikristo huku Uislamu ukishika nafasi ya pili kwa kuwa na asilimia 11.1 ya idaidi ya Watu,wengine ni Wabudha,Wahindu na Imani ya Asili huku kukiwa na Waadventista Wasabato wanaokadiliwa kuwa 600,000 nchini humo.

Unknown

Author & Editor

Naitwa Prince Emanuel, ni mtangazaji na muandaji wa vipindi kupitia Morning Star Radio na Morning Star Televesion Tanzania.

1 comments:

  1. HAPA KAAZI TU.....MAGUFULI WA HUKU...JE TANZANIA MWAFATA MKONDO HUU AMA PIA MWAWALAZIMISHA WANAFUNZI WA ADVENTISTE KUFIKA SHULENI SIKU YA SABATO??

    ReplyDelete

 

Copyright © UNCLE PRINCE ™ is a registered trademark.
Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.