Ad (728x90)

Tuna Develop/Design Blog & Website & Android Application ......0717331293

Friday, 21 October 2016

Filled Under:

KANISA LA WAADVENTISTA WASABATO NCHINI KUPITIA SHIRIKA LA MAENDELEA NA MISAADA - ADRA TANZANIA LIMETOA MSAADA WA SH.M46 KWA WAHANGA WA TETEMEKO LA ARDHI MKOANI KAGERA


Mkuu wa Mkoa wa Kagera meja jenerali mstaafu Salum Mstafa Kijuu,akipokea uthibitisho wa mchango wa Tsh.16M kutoka kwa Elam Bunde,Kaimu mkurugenzi wa Shirika la maendeleo na misaada la Kanisa la Waadventista wa Sabato (ADRA) Tanzania




Kanisa la Waadventista wa Sabato kupitia shirika la maendeleo na misaada ADRA Tanzania, limetoa msaada wa thamani ya Tsh. 46M kwa Mkoa wa Kagera, kutokana na tetemeko la ardhi lililotokea hivi karibuni mkoani hapa.

Akikabidhi msaada huo kwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera kwa niaba ya Kanisa, kaimu mkurugenzi wa ADRA Tanzania ndugu Elamu Bunde, amesema Kanisa limeguswa sana na tatizo walilopata wananchi wa Kagera na kuongeza kuwa Kanisa litaendelea kuunga mkono jitihada za Serikali ili kuhakikisha maisha ya wahanga wa tetemeko yanarudi katika hali ya kawaida.

Akipokea msaada huo mkuu wa Mkoa wa Kagera meja jenerali mstaafu SALUMU MUSTAFA KIJUU, amelishukuru kanisa la Waadventista wa Sabato kwa kuwa mstari wa mbele kwakutoa na kuongeza kuwa hiyo ndiyo dini ya kweli. Kijuu ameongeza kuwa Mkoa wa Kagera bado unahitaji msaada mkubwa kutokana na athari kubwa zilizojitokeza katika miundombinu ya huduma za kijamii kama barabara, shule na hospitali.

Aidha mkuu wa Mkoa amezitaja baadhi ya athari hizo kuwa ni pamoja na vifo vya watu 17, majeruhi 440 kati ya hao 23 wamefanyiwa upasuaji mbalimbali kutokana na kuvunjika baadhi ya sehemu za miili yao. Katika tetemeko hilo jumla ya majengo 2072 yalianguka kabisa, 16595 yamepata mipasuko hatarishi na hayafai kukaliwa na watu na jumla ya nyumba 9927 zimepata mipasuko inayoweza kutengenezwa.

Hata hivyo KIJUU hakutaka kufafanua juu ya kiasi gani cha fedha kiliingizwa kwenye akaunti bandia ya maafa iliyofunguliwa kinyume na utaratibu wa serikali na baadhi ya watumishi wa mkoa kwa madai kuwa jambo hilo liko mahakamani. KIJUU ameongeza kuwa wananchi walioathirika wanapaswa kuanza kukarabati nyumba zao kwakuwa serikali itaanza kukarabati miundombinu ya huduma za jamii kama barabara, shule na hospitali.

Kwa mujibu wa taarifa ya mkuu wa mkoa, tadhimini iliyokwisha kufanyika, zinahitajika Tsh 10 billion kurejesha miundo mbinu ya huduma za kijamii katika hali yake ya kawaida na 880 bilion kujenga nyumba 16,595 zilizo athirika mkoani hapa.

Mkoa wa Kagera ulipata tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 5.9 kipimo cha richter lililopiga chini umbali Wa km 40 Sept 10, 2016 na kupelekea vifo vya watu 17, kubomoa nyumba 2072 na jumla ya majengo 16595 kuharibiwa vibaya na hivyo Serikali kuutangaza Mkoa wa Kagera kuwa Mkoa wa maafa unaohitaji msaada wa dharula.

Unknown

Author & Editor

Naitwa Prince Emanuel, ni mtangazaji na muandaji wa vipindi kupitia Morning Star Radio na Morning Star Televesion Tanzania.

0 comments:

Post a Comment

 

Copyright © UNCLE PRINCE ™ is a registered trademark.
Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.